Thursday, March 26, 2009

UTAMBULISHO WA BLOG MPYA

Wasichana ndio wanaopambana na changamoto nyingi tofauti na wavulana

Kama nilivyoeleza hapo juu kuwa blog hii ya Behavefree ni blog itakayokuwa inajadili tabia mbali mbali za vijana ikiwa ni moja ya changamoto zinazowakabili vijana katika kufikia malengo yao ya baadaye katika jamii.

Je kutokana na changamoto hizo wamewezaje kubadili tabia zao na kufikia malengo yao na hatimaye kupata mafanikio katika kuendesha maisha yao?

Blog hii itakuwa ikitafuta majibu ya maswali yote yanayowahusu vijana hapa nchini. Pia kutakuwa na habari za kuchangamsha, kufurahisha na kuelimisha.

Hapa nitakuwa nikiibua mijadala mbalimbali, ambayo itakuwa ikiwasaidia vijana kutafakari upya mustakabali wa maisha yao kutokana changamoto zinazowakabili katika masuala ya elimu, ujasiriamali, siasa, na maisha kwa ujumla.

Natumaini nitapata ushirikano kutoka kwa wanablog wenzangu walionitangulia katika uwanja huu wa blog pamoja na wasomaji kwa ujumla.

Natarajia kupata ushirikianao wenu.

16 comments:

Mzee wa Changamoto said...

Karibu saaana Dada Digna. Karibu sio kwa kuwa umeanzisha blog, kwa kuwa umeingia katika HATUA ZA UKOMBOZI HALISI ambao unapaswa kutuhusisha sisi vijana na kwa ajili ya jamii na hasa vijana.
Umekuja na changamoto nzuri na naamini tutakuwa bega kwa bega katika kusaidia. Kama ulivyosema kuwa ni msomaji wa CANGAMOTO YETU BLOG hivyo naamini umekutana na "watafakarishaji wengi" ambao kwa pamoja (kama familia) tunaendeleza kazi hii ya kuyatambua matatizo yetu na kujaribu kuyatatua. Karibu kujiunga nasi na licha ya mimi binafsi kukuweka kibarazani pale kwa utambulisho, naamini utapita na kwao "kugonga hodi"
Kila penye uhitaji wa msaada basi usisite kufanya hivyo kwani kila umuonaye hapa alisaidiwa na (naamini) yuko tayari kusaidia.
Ndilo lengo la kuwa pamoja.
PAMOJA DAIMA

Anonymous said...

Karibu sana.

Yasinta Ngonyani said...

Digna karibu sana katika yote nami nasema te TUPO WOTE

Koero Mkundi said...

Hata mimi nakukaribisha bibie,
Karibu sana jumuiya hii ya wanablog, naamini kuna mengi utatufunza na pia tutajifunza kupitia Blog yako hii ya vijana.
Tunatarajia kujifunza mambo mengi katika kibaraza hiki cha Behavefree.

Karibu sana dada yangu.

Christian Bwaya said...

Dada Digna,
Karibu sana kublogu. Uamuzi huu ni wa kupigiwa makofi na kila apendae changamoto za fikra.
Binafsi nimefarijika kwamba umekuja na mtazamo mpya. Hivyo, wadau wako tunategemea mambo mazuri zaidi, ambayo bila wewe asingewepo mwingine wa kuyajadili.

Nisiseme sana, nikukaribishe kwa mikono miwili nikikuhakikishia kuwa nimekaa mkao wa kula.

Evarist Chahali said...

Karibu sana.Inapendeza zaidi "chama" chetu kinavyozidi kukaribia mlingano wa kijinsia....tuna akina dada Koero,Yasinta,Subi,Dina,Shamim,nk na ni matumaini yangu makubwa jumuiya wa bloggers wa Kitanzania inaweza kutembea kifua mbele na kutamka bayana kuwa sauti zao zinawakilisha si tu mitizamo ya kisiasa,kijamii,kiuchumi,nk bali pia inatoka kwa jinsia zote.Gender equality at its finest!
Karibu sana!

Simon Kitururu said...

Karibu Dada Digna!Tuko Pamoja!

kamala Lutatinisibwa Lutabasibwa said...

kqaribu na ufute ugeni wa koero.

karibu kwenye hoja, vitimbi, vijenmbe na .................

nyegerage mawe kaisiki

Sophie said...

Digna,Karibu katika jumuia ya ku-blog, na binafsi nafurahi akina dada tukiongezeka (sio kwamba sipendi maendeleo ya kaka zetu!) itasaidia kupeana habari muhimu ambazo wakati mwingine zimetupita pembeni. Karibu sana na umefanya uamuzi wa busara maana utajifunza mengi mazuri na kupata uwanja wa kuelimisha.Karibu

Egidio Ndabagoye said...

Karibu sana bloguni.naomba niwasifie walio kwenye Picha.

Obat Vimax said...

nice blog and article, thanks for sharing

Meizitang Botanical said...

thanks you

poker said...

PROMO DELIMA
poker online | Agen Domino | Agen Poker|Kumpulan Poker | bandar poker | Judi Poker | bandar qiu | Judi online terpercaya

Bonus yang kami sediakan :
* TO (Turn over) sebesar 0.3% yang akan di kami bagikan setiap hari senin
* Bonus referal sebesar 10%

Ayo segera daftarkan diri anda dan bergabunglah bersama kami !!
Delimapoker.com Situs Agen Poker Online Terpercaya di Indonesia akan melayani Anda dengan profesional, memproses depo/wd dgn cepat.
Come join and be a winer with us !!

Untuk info selanjutnya silakan chat ke :
Livechat_____: delimapoker
BBM__________: 7B960959
Facebook_____: Facebook
Phone number_: +85595678845
pendaftaran___http://www.delimapoker.com/?ref=19860605

dominoqq said...

setiap orang yang ingin bermain poker online tentu saja ingin mencari situs yang terpercaya oleh karena hal tersebut kami sangat merekomendasikan anda untuk segera bergabung di situs laguqq

dominoqq said...

laguqq adalah sebuah blog review tentang situs poker online terpercaya saat ini.

dominoqq said...

Situs Bandarq Dominoqq Poker qq online terpercaya laguqq